Jumamosi, 30 Mei 2015

Waziri mkuu wa zamani Mh. Edward Lowassa ametangaza rasmi nia ya kuwania urais wa kupitia chama cha mapinduzi CCM.


Mbunge wa Monduli na waziri mkuu wa zamani Mh. Edward Lowassa ametangaza rasmi nia ya kuwania urais wa Tanzania kupitia chama cha mapinduzi mbele ya umati wa watu waliofurika uwanja wa Sheik Amri Abeid jijini Arusha na kutaja vipaumbele vyake kuwa ni elimu,kupambana na umaskini,kulinda rasilimali za nchi  na kuwaunganisha watanzania .
Mh.Lowassa ambaye aliingia.uwanjani akisindikizwa na msafara wa pikipiki na magari pia  amesema akipewa fursa atahakikisha  anadumisha muungano.
 
Amesema ataweka misingi imara ya kuharakisha maendeleo mazuri kwa wananchi  na kuwawezesha vijana kuondoa tabaka la walionacho nawasionacho.
 
Awali viongozi wa dini na siasa akiwemo kingunge Ngombale Mmwiru wameseama Lowassa ana sifa za kiongozi anayefaa kuliongoza  taifa  kwa sasa.
 
Sherehe hizo zilizohudhuriwa na maelfu ya wananchi kutoka kona mblimbli  nchini burudani kubwa  ilikuwa  ni  Helkopta ya Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Geita Bw. Joseph Msukuma.