Jumapili, 24 Mei 2015

Watanzania washauriwa kupinga mswaada wa sheria inayotaka kupitishwa na serikali ya kuzuia uhuru wa kupata habari.


Katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dk Wilibroad Slaa amewataka watanzania kupiga na kutokubali  mswaada wa sheria unaotaka kupitishwa na serikali wa kuzuia uhuru wa vyombo vya habari na kuwanyima watanzania haki na uhuru wa kupata habari.
Akiongea na wananchi mjini Bukoba katibu mkuu wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema Dk Wilibroad Slaa amewataka watanzania kutokukubali sheria hiyo ambayo inalengo la kuwanyima watanzania haki na uhuru wa kupata habari na kwamba sheria hiyo ikipitishwa watanzania wataendela kubaki gizani na kuishi kama waposhimoni bila kuelewa maovu yanayofanywa na viongozi wasio waadilifu wanaotumia madaraka vibaya kwa masalahiyao binafsi.
Hata hivyo katibu mkuu wa chama demokrasia na maendelio Chadema Dk Wilibroad Slaa amesema nia ya serikali kutaka kuzuia uhuru wa vyombo vya habari ni kuwarudisha nyuma watanzania ili waweze kuishi bila kupata habari kama ilivyokuwa enzi za ukoloni nakwamba haliyo haiwezi kuvumiliwa kwani serikali inataka kuficha maovu ambayo yanawekuliangamiza taifa hapo baadae.