Jumapili, 24 Mei 2015

TFDA yakamata vipodozi katoni 45 na maziwa Box 20 yasiyofaa kwa matumizi ya binadamu kutoka nchini Uganda.


Mamlaka ya chakula na dawa nchini TFDA imekamata vipodozi katoni 45  pamoja na maziwa yasiyofaa kwa matumizi ya binadamu Box20 vililvyokuwa vikisafirishwa kinyume na sheria katika basi la Taqwa kutoka kampala nchini uganda kwenda jijini Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya kukagua basi hilo mkaguzi wa TFDA kanda ya mashariki Dokta. Ediga Mahundi amesema  walipata tarifa za siri kutoka kwa wasamaria wema  ambapo waliweka mtego katika mzani wa Kihonda mjini morogoro na kufanikiwa kukamata vipodozi hivyo huku ameeleza  vipodozi hivyo havifai kwa matumizi ya binadamu na vimekuwa vikisababisha tatizo la watoto kuzaliwa na vichwa vikubwa na.
 
Katika hali isiyo ya kawaida  abiria waliokuwa wakisafiri kwa basi hilo wameonekana kunywa  maziwa yaliyokamatwa na mamlaka ya chakula  na Dawa wakidai maziwa hayo ni salama kwa matumizi ya binadamu na wame zitaka mamlaka husika kufanya ukaguzi wa vyombo vya usafiri kabla ya kuigia nchini.