Jumatatu, 24 Agosti 2015

CHARLES MWAKIPESILE AONGEA NA WAANDISHI WA HABARI NA KUWASHUKURU WANANCHI

Kada wa CCM  na mjumbe wa NEC, Charles Mwakipesile leo ameongea na waandishi wa habari  katika hotel ya hill view na kuweka bayana kuwa pamoja katika  kampeni na Mgombea Ubunge kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi Sambwee Shitambala. 

 Akiongelea kuhusu kukosa nafasi ya kuwakilisha jimbo la mbeya mjini amewashukuru Wananchi wa jimbo la mbeya mjini kwa kuonesha upendo kwake . na kuishukuru kamati kuu ya CCM kwa uteuzi wa shitambala.

Mwakipesile alisema  makundi yote yaliyokuwa katika kipindi cha kutafuta mgombea mmoja ndani ya chama walikaa pamoja na kukubali kwa pamoja na kufuta makundi yaliyokuwepo ndani yao.

Akiulizwa swali na mtandao huu kuhusu kukubali kwa moyo wa dhati kwa wagombea wengine  kati ya kumi waliosaini kuvunja makundi alisema kama kuna mtu ana chuki kwa sababu ya kutochaguliwa na chama atabaki na chuki yake  mwenyewe.