Jumatano, 8 Aprili 2015

TAIFA STARS YAPANGWA KUNDI LA KIFO




Safari ya kusaka tiketi ya kucheza mataifa ya Afrika mwaka 2017,yatakayo fanyika nchini Gabon timu ya taifa Taifa stars wamewekwa kundi G sambamba na Nigeria pamoja na Misri.

Katika miaka ya hivi karibuni timu ya Taifa stars hawajawi kucheza na Nigeri katika michezo ya aina yoyote ile, wakati timu za taifa za vijana ya Nigeria imekuwa ikizisambaratisha timu za vijana za Tanzania kila wanapo kutana.

Kipindi cha Maximo na Jan Poulsein Taifa stars imewahi kucheza michezo ya kirafiki na Misri, ambapo katika michezo hiyo wamekuwa wakifungwa goli si chini ya 5.

Nigeria na Misri hawajashiriki michuano iliyopita ya mataifa ya Afrika ikiwa ni mara ya tatu mfululizo kwa Misri kuyakosa michuano hiyo mikubwa ya Afrika.