Jumamosi, 25 Aprili 2015
KUELEKEA MCHEZO WA LEO MWABUSI ANENA KUHUSU KUWAKOSA WACHEZAJI WAKE WATATU
Kikosi cha Mbeya City Fc leo kinashuka kwenye uwanja wa Sokoine kusaka pionti tatu muhimu mbele ya Kagera Sugar kutoka Bukoba mkoani Kagera kwenye mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara huku ikiwakosa nyota wake watatu Steve Mazanda na Yusuph Abdalah walio majeruhi pia Themi Felix anayetumikia adhabu ya kadi nyekundu.
Akizungumza kuelekea mchezo huo Kocha Mkuu wa City, Juma Mwambusi, amesema licha ya kuwakosa nyota hao amekiandaa vizuri kikosi chake kwa lengo la kuibuka na ushindi katika mchezo huo akiwa na hesabu za kusogea juu kwenye msimamo wa ligi.
“Nimewaandaa vizuri wachezaji wangu, lengo letu ni kushinda ili tupate pointi tatu ambazo zitatusogeza juu kwenye msimamo, nitawakosa Themi,Mazanda na Sisalo lakini sina shakana hilo, kwa hesabu za haraka najua mchezo huu utakuwa mgumu kwa sababu tunaihitaji nafasi ambayo wapinzani wetu wapo na wao bado wanahitaji kubakia walipo ni wazi mchezo utakuwa na ushindani mkubwa lakini nina imani tutaibuka washindi” alisema.