Jumamosi, 25 Aprili 2015

WASAUZI WAANZA KUOGOPANA WAO KWA WAO

Raia wagopana Afrika KusiniHuku hali ya amani ikianza kurudi katika baadhi ya mitaa iliyogubigwa na vurugu za kupinga na raia wa kigeni nchini Afrika Kusini imeelezwa kuwa raia wa nchi hiyo wanaogopana wenyewe kwa wenyewe.
Baadhi ya raia walipohojiwa na BBC, moja ya ripoti zilizoruka kwenye kipindi cha Amka na BBC walisema pamoja na hali kutulia lakini kwenye mizunguuko na shughuli zao za kila siku kila mmoja anamuogopa mwenzake. “Huwezi kumuamini hata jirani yako”, alisema mmoja wa wahojiwa.
Nchi ya Afriaka kusini ilikumbwa na ghasia zilizosababisha watu kadhaa kufariki huku raia wapatao mia tatu kukamatwa kwa kusababisha vurugu kwa raia wakigeni.
Takwimu zinaonyesha Afrika Kusini inaidadi ya wageni wapatao milioni mbili sawa na asilimia nne ya watu wote wa nchi hiyo.
Tangu juzi kumeanza kufanyika maandamano ya amani kupinga vitendo hivyo, vilivyoitia doa nchi ya Afrika ya Kusini kwa mataifa mengine.