Jumatano, 22 Aprili 2015

KATIBU MKUU WA CHADEMA AWASILI NCHINI JANA

harubutz.blogspot.com

Ni mapokezi ya katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Willibrod Slaa akitokeaa nchini Marekani ambapo alipata mwaliko kutoka kwa Gavana wa Jimbo la Indianaambapo pia ni meya wa jiji la Indianpolice lilipo katikati kidogo ya Marekani mwaliko ambao uliambatana na mwaliko kutoka vyuo vikuu vinne ambao mwaka mmoja na nusu vyuo hivyo vilishawai kutuma mwaliko kwa chama hiki .
Akielezea ni jinsi gani alivyoweza kutekeleza dhana ya hakuna kulala kwa vitendo kwani ameweza kutembea umbali mrefu akiwa angani mwendo takribani wa masaa ishirini na tatu, Huku akielezwa kufarijika na mapambano yanayoendelea ya kutafuta uongozi pia alieleza kuona picha nyingi na kupata habari kutoka katika mitandao ya mapambano na kupongeza zinduzi wa mafunzo ya viongozi na wenyeviti wa serikali ya mitaa uzinduzi uliofanyika katika uwanja wa sabasaba PTA wiliya ya Temeka jijini Dar es Salaam.
Huku akisema katika zihara yake wenyeji wake walishangazwa na picha ambazo zilionyesha vikao vya CHADEMA ambavyo vimeudhuriwa na wanachama wengi kitu ambacho aliweza kuewaeleza kuwa ni moja ya dhamira ya watanzania kutaka kufanya mabadiliko na sio mjini tu mpaka vijijini hali ni hiyohiyo.
Akieleza mambo aliofanya akiwepo katika zihara hivyo Dr Willbrod Slaa misingi ya zihara ni kwenda kuimarisha mauhusiana mahusiano baina ya CHADEMA na serikali ya jimbo la Indiana, Akifafanua maana halisi ya jimbo Dr Slaa amelielezea kuwa jimbo ni kama Nchi ambapo kule huita STATE.
Huku akiwakumbusha wananchi na wanachama waliojikoze kwenda kumpokea kuwa dhana ya chadema katika chaguzi zilizopita ilikuwa na sera ya kuunda majimbo swala ambalo wenzetu ndio wamelitekeza na kuleta mafanikio makubwa sana katika eneo husika la kila jimbo.akisisistiz akusema mfumo wa jimbo ni kila jimbo huwa na kiongozi wake na serikali yake hivyo jambo ambalo kila serikali ya eneo husika hupikagia maslahi na msukumo wa maendeleo.
Akielezea umuhimu wa mausiano hayo Dr Slaa alisema mahusiano hayo ni kwasababu anajua chadema inakwenda kushika Nchi na ndio maana chadema husisitiza mausiano na nchi ambazi zitakwenda kushirikiana nazo ambapo ikiwa madarakani na kusisitiza kusema Marekani kila jimbo linaweza kutengeneza mahusiano na nchi yoyote  bila kuishikisha serikali kuu.
Akilielezea jimbo la Indiana ambalo miaka thelasini iliyopita ilikuwa ni maskini na ilikuwa ikijishughulisha na maswala ya kilimo na ufugani lakini leo hii nchi hiyo imeweza kuwa ni nchi inayosimamia katika maswala ya viwanda na kilimo na ufugaji wa kisasa. Dr Slaa alisema alipokuwa Indiana alifanikiwa kutembele shamba la ufugaji lenye ngombe elfu kumi ambapo kila ngombe mmoja hukamuliwa lita 135 jambo ambalo hata kwetu Tanzania linawezekana ikiwa serikali itasimamia kikamilifu suala ya ufugaji na kilimo kicho sahihi kwa kuwawezesha wakulima na wafugaji huku akishangazwa na upotevu wa malighafu nyingi kupotea zitokanazo na ufugaji kama vile ngozi, kwato pamoja na pembe.
Akiwaeleza wanachama na wananchi waliojitokeza kumpokea kuwa Watanzania wamekalia Dhahabu na kueleza anapo zungumzia Dhahabu hamanishi madini pekee yake ila ni pamoja na uwanja wa ndege pamoja na bandari, Huku akiufanananisha uwanja wa ndege wa jijini Dar es Salaam kuwa ni mara kumi ukiuliknganisga na uwanja wa ndege wa Indiana. Akisisitiza kusema ni aibu kubwa sana kukuta ndege mbili jambao ambalo ni aibu kwa taifu na inaonyesha dhahiri kuwa nchi imekufa kiuchumi kwani alipokuwa kaibadilisha ndege akiwa Qatar alipanda ndege yenye uwezo wa kubeba watu mia mbili lakini ndege hiyo hakuwa ha tan a watu hamsini hii inaonyesha dhahiri kuwa nchi umeshuka kiuchumi.
Huku alisisitiza kusema CHADEMA haina ugomvi na wawekezaji kwani Nchi zinazoendelea laziwa ziwe na wawekezaji lakini ugomvi wa CHADEMA ni kwa wawekezaji mafisadi ambao wanaingia mikataba ya siri na serikali kwa maswahi yao binafsi, Huku akieleza mafanikio ya Nchi za wenzeku kuwa ni kuwa hivyo basi tunaitaji mambo muhimu kutoka kwao ili kuweza kuleta msukumo katika maendeleo ya NChi kama vile technologia, elimu pamoja na nyenzo hivyo ni vitu ambavyo vinaleta msukumo wa maendeleo katika Nchi.
Akigusia swala la elimu kutoka kwa Nchi za wenzetu Dr Slaa ameeleza kuwa vyuo vya wenzetu huzalisha wataalamu na kuwatumia tofauti na vyuo vyetu ambavyo vimekuwa ni sehemu ya kuchukulia vyetu na kuwaacha wataalamu wetu wakiwa wanazagaa mitaani jamabo ambalo huwezi kulikuta kwa wenzetu.
Akitolea mfano wa mabadiliko ya vyou ambavyo vilikuwa nu vyuo vya professional na badala yake kuvifanya kuwa vyou vikuu jambo ambalo limeshusha utendaji katika jamaa kwani vyuo vikuu huzalisha academic na professional huzalisha watendaji jambo ambalo wenzetu wamebakisha vyuo vyao vya professional kubaki kuwa hivyo hivyo na vyuo vikuu kuwa ni vyou vya kuzalisha academic.
Akijibu swali kutoka kwa mwandishi wa habari swali ambalo alimuliza Dr Slaa anatoa kauli gani kutokana na serikali kushindwa kukamilisha mchakato wake wa kura za maoni ya katiba na swala la uwandikishaji kwa mfumo wa BVR, akijibu swali hilo Dr Slaa ameelza kuwa ameshaliongelea swala hio na kuwataka serikali hususana Kikwete kumalizia uongozi wake kwa usalama na kuiacha Nchi kama alivyoikuta asijaribu kuiingiza Nchi katik machafuko na wala asijaribu kuhairisha uchaguzi kwani ndio swala kubwa litakalo pelekea Nchi katika machafuko.Akisisistiza kusema katika zihara yake Nchi Marekani hawatumii BVR na kusema BVR ni ufisana kwani na kuwakumbusha kwa waliofatilia swala hili tenda ya BVR ilikataliwa na Mamlaka na ununuzi wa umma na baada yake wakaipitisha kinyemela lengo kuu ni kutaka kupunguza wapiga kura na ndio maana walianza kuwaandikisha sehemu ambazo wanaamini kuwa ni ngome ya CCM. Akitoa tamko Dr Slaa la kusema pamoja na Tume kuwa na mapungufu yake lakini tayari walishakaa na Kikwete tarehe 31/8/2014 na kukaa tena tarehe 8/9/2014 na kukubaliana kupunguza mzigo kwa serikali kwa mambo amabyo sio lazima kwa mfano kura ya maoni sio jambo la lazima sio swala la kikatiba ila ni swala la kisheria na kumtaka kuelekeza fedha katika serikali za mitaa amabayo ni maandalizi ya kuawaandikisha wapikagaru ambapo tukielekea uchaguzi mkuu.
Akisisitiza kusema Raisi alipendekeza kwa mdomo wake na kama ni uwongo atoe kauli ya kudhibitisha kuwa swala hilo ni la uongo ambaye yeye ndio aliyesema tutaahirisha zoezi la kupiga kura hadi uchaguzu nkuu ili kuokoa fedha lakini baadae akageuka na kutangaza tarehe jamabo ambalo halikuwa katika mamlaka yake, sasa tuonaona serikali ilivyotumia fedha nyingi sana katika kufanya kampeni na kufanya mchakato mzima katika jamabo hillo ambalo leo hii limeishia njiani.
Akijibu swali la pili kutoka kwa mwandishi wa habari mwingia aliyeuliza ni nini tamko la chadema au ni maamuzi gani wanataka kuyachukua juu ya serikali katika utumiaji mbaya wa fedha za umma au ni kwenda Mahakamani, Kijibu swalli hilo Dr Slaa aliwaeleza kuwa chadema haina mpango wa kwenda mahakamani kwani kuna kesi nyingi ambazo bado hazijasikilizwa.
Akijibu swali la nyongeza ambalo limeuliza anatoa kauli gani juu ya mauwaji yanayoendelea south afrika
Dr Slaa alisikitisha na mauuwaji hayo na kuitaka serikali kutolea tamko nini maana ya ubalozi wa Tanzanio kazi yake uliopo Nchini Afrika ya kusini na kuinya Tanzania kuwa yanayotokea Afrika ya kusini ni matokeo ya serikali kushindwa kuwapatia wananchi wake mambo muhimu hivyo sio ajabu na hapa Tanzania ikatokea machafuko ya aina hiyo.