Jumanne, 21 Aprili 2015

YANGA YASEMA LEO ITAENDELEZA DOZI KATIKA UWANJA WA TAIFA DHIDI YA STENDI UNITED

 

Vinara wa ligi kuu ya vodacom Yanga leo wanataraji kuwa wenyeji wa Stand United ya Shinyanga katika muendelezo wa ligi kuu ya vodacom, mchezo utakao chezwa katika uwanja wa Taifa.

Mchezo wa leo ni muhimu kwa yanga kama wanataka kutangaza ubingwa wa Tanzania bara kabla ya kwenda kuwavaa wa Tunisia Etoil Du Saheil katika mchezo wa marejeano utakao fanyika nchini Tunisia.

Nayo stand unite inayokabiliwa na michezo miwili migumu katika juma hili, watakuwa wanahitaji pointi tatu kujinusuru kutoshuka daraja, kutokana na kuwa na pointi 38 ambazo zinawezwa kufikiwa na Polisi Morogoro mwenye pointi 24 akiwa katika nafasi ya pili kutoka mwisho na Tanzania Prisons aliye katika nafasi ya mwisho, akiwa na pointi 22.

Katika mchezo wa leo huenda tukashuhudia urejeo wa Mbrazili Andrew Countinho aliyekosekana kwa majuma 10 kutokana na majeraha aliyokuwa nayo, sambamba na kiungo anae tamba kwa sasa Salum Telela, aliyekosa mchezo dhidi ya Etoil Du Saheil kutokana na majeraha.

Endapo Stand unied wakifanikiwa kuondoka na pointi hii leo katika uwanja wa Taifa, kutapeleka matumaini Chamanzi, makao makuu ya Azam FC, ambao wanahamu ya kuwa timu ya pili nje ya Simba na yanga kutetea ubingwa wa ligi kuu ya vodacom.

Mkuu wa kitengo cha habari wa yanga Jerry Muro akizungumza na moja ya kituo cha redio hapo jana alijinasibu timu yake ya yanga itaibuka na ushindi wa goli 10 hi leo.

Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza yanga walifanikiwa kuibuka na ushindi wa goli 3-0 katika uwanja wa CCM Kambarage.

Na hii inakuwa ni kwa mara ya pili Stand united kucheza mchezo wa ligi kuu katika uwanja wa Taifa ambapo mchezo wake wa kwanza walifanikiwa kutoka sare ya kufungana goli 1-1 dhidi ya Simba SC.

Kocha wa Stand united alijinasibu kufanya vyema katika mchezo wa leo hapo jana pale alipokuwa akihojiwa na moja ya redio nchini, hku akiwategemea zaidi Chanongo na Mnigeria katika kupeleka zaama katika mitaa ya jangwani hii leo.