Ijumaa, 8 Mei 2015

JUMA NYOSO OUT MCHEZO WA KESHO NA POLISI




Mlinzi wa kutumainiwa wa Mbeya City Fc, Juma Nyosso ataukosa mchezo wa mwisho wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara dhidi ya Polisi Morogoro unaotarajiwa kuchezwa kesho jumamosi kwenye uwanja wa Sokoine kufuatia kadi tatu za njano  alizoonyeshwa kwenye michezo iliyopita.
Akizungumza    kocha mkuu wa mbeya city Juma Mwambusi amesema kuwa  Nyosso  alipata  kadi za njano tatu mfululizo kwenye michezo iliyopita  hivyo ni wazi hatakuwa sehemu ya kikosi jumamosi hii.
“Nahodha wetu (Nyosso) ataukosa mchezo  wa jumamosi hii ni kutokana na  kadi  tatu za njano, alipita mfululizo kwenye michezo iliyopita, ni pigo  kumkosa  kwenye mchezo muhimu kama huu lakini hatuna wasiwasi kwa sababu tayari tushaandaa  vijana wengine  kuziba pengo lake na imani yangu kubwa watafanya kazi nzuri” alisema.
Kuhusu mchezo wa jumamosi kocha  Mwambusi amesema kuwa  maandalizi  kuelekea mchezo huo yamekamilika kinachosubiriwa ni siku ya mchezo tu  City iingie uwanjani kutafuta matokeo.
“Kwetu sisi kila kitu kimekamilika, tunasubiri siku ya mchezo  tu, hizi zitakuwa dakika 90 zingine muhimu kwetu kwa sababu tunahitaji matokeo ili kusalia kwenye nafasi ya nne, hili linawezekana, tulianza ligi vibaya lakini tukaweka malengo ya kumaliza kwenye nafasi tano za juu na hili  litatimia”  alimaliza.