Alhamisi, 16 Aprili 2015

USIKU WA ULAYA: BARCELONA YAITIKISA PSG NYUMBANI




Kwenye usiku wa Ulaya jana michezo miwili ilichezwa katika hatua ya robo fainali ambapo FC Porto ya Ureno waliwakaribisha Bayern Munich ambapo mchezo huo ulimalizika kwa Bayern Munich kukubali kichapo cha 3-1.
Huko nchini Ufaransa pia Paris Saint German ilikuwa mwenyeji wa miamba ya soka ya Hispania Barcelona ambapo mchezo huo ulimalizika kwa PSG kukubali kichapo cha 3-1 katika uwanja wa nyumbani.
Magoli ya Barcelona yalitiwa nyavuni na Neymar Jr huku Luis Suárez akiziona nyavu za PSG mara mbili magoli yaliyoiweka timu hiyo kwenye nafasi nzuri kusonga mbeleTimu zote nne zitacheza michezo ya marudiano April 21 siku ya Jumanne.