Jumatatu, 20 Aprili 2015

FORMULA 1: LEWIS HAMILTON ATWAA TAJI LA BAHRAIN GRAND PRIX


Lewis Hamilton atwaa taji la Bahrain Grand Prix kwenye mbio za magari za Formula 1 (Langalanga).
Katika mchuano huo Hamilton amewabwaga wapinzani wake Kimi Raikkonen na Nico Rosberg kuhakikisha anaongoza na kutwaa taji hilo.
Ushindi huo kwa dereva huyu wa raia wa Uingereza ni watatu katika msimu huu akiitumikia vyema kampuni ya Mercedes huku akimuacha dereva mwenzake kutoka kampuni hiyo Nico Rosberg akishika nafasi tatu baada ya kubwaga na Kimi Raikkonen kutoka kampuni ya Ferrari
Kwa matokeo hayo aliyoyapata dereva huyu mwenye mafanikio kwa sasa unamuweka kwenye rekodi nzuri ya mbio za magari za Formula 1