Jumanne, 24 Novemba 2015

KIKOSI CHA MBEYA CITY KINAENDELEA NA MAZOEZI HUKO TUKUYU MBEYA

DSC_0006
KIKOSI kamili cha Mbeya City Fc kinaendelea na mazoezi  kwa ajili ya kujiweka sawa tayari kwa mzunguko wa pili wa ligi kuu ya soka Tanzania bara  unatarajia kuanza ‘kutimua vumbi’ desemba 12  huku City ikipangwa kuanza na Mtibwa Sugar kwenye uwanja w Sokoine jijini Mbeya.
Mapema leo  kwenye kambi ya City iliyopo chuo cha ualimu Tukuyu jijini hapa kocha mkuu Meja mstaafu Abdul Mingange ameuambia mtandao  huu kuwa  hali ya mazoezi yaliyoanza  jumapili iliyopita ni nzuri kwa  sababu wachezaji mwitikio wa wachezaji kuwahi kambini kama iliyokuwa imepangwa  umekuwa mzuri hivyo  kurahisisha  programu zake kwenda vizuri.
“Mwitikio wa wachezaji kuwahi kambini umekuwa mzuri, hii imerahisisha  sana programu zangu kwenda sawa mpaka sasa ni wachezaji  20 wameshafika hapa hivyo hali ni nzuri, kikosini wanakosekana  Juma Kaseja, Haruna Moshi na Haruna Shamte ambao walikuwa na ruhusa maalumu na ninawatarajia watakuwa hapa baada ya siku mbili” alisema.
Akiendelea zaidi Mingange aliweka wazi kuwa ameamua kuanza kambi mapema ili kuhakikisha kikosi chake kinakuwa kwenye hali nzuri kabla ya kuivaa Mtibwa Sugar desemba  12 kwenye uwanja wa Sokoine  huku akiweka matumaini ya kupata matokeo mazuri kwenye michezo ya mzunguko ujao kufuatia  anguko la  awamu ya kwanza.