Jumamosi, 18 Julai 2015

Homa yazidi kupanda kwa watangaza nia Ubunge Mbeya Mjini James Mwampondele Achukua Fomu ya Ubunge


Mdau mkubwa wa michezo Mkoani Mbeya James Mwampondele amechukua  Fomu ya  kuomba kupata Ridhaa ya ubunge kupitia chama chake katika ofisi za ccm wilaya ya mbeya mjini moja ya Matukio makubwa ambayo ameyafanya  mwampondele ni  kujitolea kutengeneza magoli ya Netball katika viwanja mbalimbali vya shule za msingi vilivyopo jijini mbeya .ameweza kutoa msaada mkubwa wa kutengeneza uwanja wa sokoine kwa kupanda nyasi na gari lake kutoa nyasi toka Tukuyu na kuwezesha uwanja wa mpira kutumika katika michezo ya ligi kuu tanzania bara amekuwa ni mmoja wadau wakubwa wa kuchangia maendeleo  ya vijana mmoja mmoja na vikundi mbalimbali ,ikiwemo kusaidia Kwaya mbalimbali za dini ,kusaidia sanaa kwa upande wa waigizaji ,mpira wa miguu kuzipatia jezi timu  mbalimbali za jijini mbeya ikiwemo  mipira ya miguu na netball.hata hivyo alisema endapo hata pata ridhaa ya kuchaguliwa na chama chake na baadae kupata nafasi ya  kuchaguliwa na wananchi kuliongoza jimbo la mbeya mjini Atahakikisha  anafuata Ilani ya chama cha mapinduzi  (CCM) na kuweza kuwasaidia wakazi wa jimbo la mbeya mjini kuwawezesha  kupata Elimu ya kuendesha biashara ndogo ndogo na kuweza kuwafungulia Saccos za kuwakopesha  vitu au pesa ili kuweza kuondokana na Tatizo la umaskini katika jimbo la mbeya mjini.