Ijumaa, 15 Mei 2015

MAPINDUZI YAFELI BURUNDI



 





 

Mnamo 13 mwezi May jenerali mmoja wa jeshi alitangaza katika redio ya taifa kwamba rais wa Burundi amepinduliwa na kwamba serikali ya mpito itabuniwa.Lakini msemaji wa rais alikana habari hizo akidai kuwa kulikuwa na usaidizi mdogo katika jeshi kwa mapinduzi kutendeka.

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ameonya kuwa atalipiza kisasi dhidi ya mtu yeyote ambaye atashambulia Burundi.''katika taarifa yake amesema kuwa ''hatutakubali mtu yeyote kuwasha moto Burundi''.

Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza ametuma ujumbe katika mtandao wake wa tweetter kwa lugha ya kirundi akisema kuwa ''Nilifurahi kuona vile raia wa Burundi walivyonipokea katika mji wa Bujumbura pamoja na mikoa mingine

Kuna mazingira ya hofu na switofahamu katika mji wa Bujumbura kufuatia kufeli kwa jaribo la mapinduzi kulingana na mkaazi mmoja wa mji huo.Serge Ntabikiyoboka anasema kuwa hadhani kwamba taifa hilo literejea katika hali yake ya kawaida hivi karibuni.

Tume ya haki za binaadamu katika umoja wa mataifa imeonya kuhusu ulipizaji kisasi kufuatia jaribio la mapinduzi nchini Burundi.Msemaji wake Rupert Coleville amesema kuwa tume hiyo ina wasiwasi kuhusu matukio ya taifa hilo katika kipindi cha siku mbili zilizopita.