Jumanne, 21 Aprili 2015

CHADEMA WAZINDUA MAFUNZO KWA WENYEVITI WA MITAA DAR ES SALAAM


MH FREEMNA MBOWE AKITOA TAKWIM YA WAPIGA KURA JIJI LA DA ES SALAAMUzinduzi wa mafunzo ya viongozi na wenyeviti serikali ya mtaa ulifanyioka katika ukumbi wa PTA wiliya ya Temeke jijini Dar es Salaam, uzinduzi wa mafunzo hayo ambayo yalifunguliwa rasmi na mwenyekiti Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA( Mh Freeman Mbowe aliwataka viongozi hao na wenyeviti wa serikali za mitaa kuwa makini na kufata kanunu za uongozi kwa kuwa na maadili safi kwani dhamana waliyopewa na wanancho wao sio nafasi ya kufanya mchezo. Pia akitumia mkutano huo kuwapongeza wale wote waliochaguliwa kuongoza serikali za matiaa na kuwataka wafanye kazi kikamilifu katika ofisi zao kama ilivyoonekana kupata mafanikio katika manispaa ya kinondoni kwa kuongozwa na madiwani wa chadema jambo ambalo limeweza kuongeza kipato cha manispaa hiyo. Akimtaka Naibu katibu Mkuu wa Bara Mh John Mnyika kutaja takwimu la ongezeko hilo la ukusanyaji wa fedha jambo ambalo Mh John Mnyika alimwita mwenyekiti wa Madiwani manispaa ya kinondoni Mh Rosse Mushi na kueleza ongezeko la kipato hicho kutoka Billioni Saba mpaka kufikia Billioni thelasini na tano, huku pato la ndani ukijumlisha na mgao kutoka Serikali kuu ni shillingi Millioni saba na kwasasa kufikia Billioni moja themanini na nne. Akisisitiza kutoridhishwa na ongezeko hilo Mh John Mnyika aliwataka viongozi na wenyeviti wa serikali za mitaa kuhakikisha wanaongeza nguvu kuhakikisha manispaa zinaongozwa na chadema na meye pia na wabunge ili kuweza kuzibiti kipato cha manispaa kikamilifu.
Mh Freeman Mbowe alieleza kuwa kipato cha Taifa kinategemea mkoa wa Dar es Salaam ukiachilia mbali makao makuu ya serikali kuwa katika jiji hili na ofisi nyingine nyeti kubwa, Akibainisha hayo pia alieleza idada ya wapiga kura ambao ndio wanaipa dhamana chama gani kinachoweza kuongoza Taifa na kuwaeleza kwa wingi za wapiga  kura wa mkoa wa Dar es Salaam ndio wenye dhaamana hiyo ya kuchagua chama gani kiongoze nchi.
akianza kutaja idadi ya wapiga kura alieleza jimbo la ubungo ndio linalooongoza kuwa na wapiga kura wengi laki tano elfu sabini na tano mia tatu sitini na sita, jimbo la pili ni jimbo la kigamboni lenye wapiga kura laki nne elfu sabini na nane na thelasini, jimbo la tatu ni jimbo Temeke lenye wapiga kura laki nne elfu kumi na saba mia nne na thelasini na mbili, Jimbo la tatu ni segerea lenye wapiga kura laki nne elfu kumi na moja mia sita na ishirini, Jimbo la nne ni jimbo la Kawe lenye wapiga kura laki tatu elfu mia nne na themanini na tatu. jimbo la tano ni Kinondoni lenye idadi ya wapiga kura laki tatu elfu mia sita na sabini na nane. na jimbo la Ukonga lenye wapiga kura laki mbili elfu selasini na tisa mia tatu na sabini na tano.
Akawaeleza nini maana ya takwim hizo ni kwamba idadi ya wapiga kura wa mkoa wa Dar es Salaam ndio itadi kubwa kuliko mkoa wowote hivyo ni muhimu kufanya kazi na kutengeneza mazingira mazuri ya ushindi tunapoelekea uchaguzi.