Jumatatu, 13 Juni 2016

MASHINDANO YA KIMONDO CUP YAFUNGULIWA RASMI


Mashindano ya Kimondo Cup hatimaye yamezinduliwa siku ya Jana katika uwanja wa mlangali wilayani mbozi Mkoa wa Songwe. Akitoa risala fupi Mh. Diwani wa kata ya mlangali ambaye pia ni Mwenyekiti wa halimashauri ya Mbozi Erick Ambakisye alisema mashindano hayo yamekuwa na changamoto nyingi ikiwemo uendeshaji wake umekuwa mgumu Sana ukizingatia mashindano hayo hayana mdhamini.lakini pia alisema faida ya mashindano hayo yameonekana kwa kipindi kilichopita cha miaka miwili kwa kutoa wachezaji kwenda ligi kuu .akiwemo Geofrey mwashiuya anaikipiga timu ya yanga na Geofrey mlawa anaekipiga mbeya city. Naye mgeni rasmi wa ufunguzi wa kimondo cup mkuu wa wilaya ya mbozi mkoa wa songwe mh.Ahmad alisema kwa upande wa serikali itashirikiana kuwasaidia kujenga mahusiano na makampuni ili waweze kudhamini mashindano hayo.

Pamoja na hayo ulipigwa mchezo wa ufunguzi wa mashindano hayo Kati ya mabingwa watetezi wa msimu uliopita wembe fc waliofanikiwa kushinda mchezo huo kwa magoli 2 kwa 1 dhidi ya haterere fc mashindano haya yanatarajia kuanza kesho katika viwanja mbalimbali wilayani mbozi Kata ya mlangali.

Mabingwa watetezi wa Kimondo Cup Wembe Fc wakiwa katika picha ya pamoja kabla  mchezo kuanza wa ufunguzi.