Jumatatu, 13 Juni 2016

UVCCM MKOA WA MBEYA NA SONGWE WATOA TAMKO LA KUMUUNGA MKONO NAIBU SPIKA DR. TULIA ACKSON


Mwenyekiti wa Uvccm mkoa wa mbeya na songwe Aman kajuna ametoa tamko la Umoja wa vijana (UVCCM) la kumuunga mkono mh. Dr. Tulia Akson Naibu spika wa bunge la jamuhuri ya muungano wa tanzania .Akisoma risala mbele ya waandishi wa habari alisema wanasikitishwa na kulaani vikali na vitendo vinavyofanywa na wabunge wa upinzani vya kutaka kumhujumu naibu spika kwa sababu zao binafsi zisizo na maslahi kwa umma isipokuwa kwa vyama vyao pekee kwani uwezi kumuondoa naibu spika kwa kusimamia kanuni na taratibu zilizotungwa na wao wenyewe waheshimiwa wabunge na kuwanyima wananchi waliowachagua .Rai yao kwa wapinzani Wanawashauri wapinzani kurejea maneno ya busara yaliyotolewa na Dr. Harrison Mwakyembe. UVCCM imewaomba wabunge wa upinzani walejee bungeni kuwawakilisha wananchi waliowachagua kwa kuwatetea kwa hoja za msingi zenye maslahi kwa taifa na sio vyama vyao Pekee.