Jumatano, 8 Aprili 2015

MBEYA CITY YAILAZIMISHA AZAM SARE






Wagonga nyundo wa jijini Mbeya, Mbeya city hii leo wameikomalia Azam Fc na kufanikwa kwenda nayo sare ya kufungana goli 1-1 katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa Azam complex.
.
Katika mchezo wa leo  timu zote zilienda mapumziko zikiwa bado hazijafanikiwa kuona nyavu za mwenzake.
Azam FC walikuwa wa kwanza kupata goli kupitia kwa Kipre Bolue katika dakika ya 61 kabla ya Mbeya city kusawazisha kwa mkwaju wa penati uliopigwa na Rafael alpha na kupelekea mchezo kumalizika kwa sare ya kufungana goli moja moja.

Mchezo huo ni mchezo wa pili mful;ulioz katika uwanja wa Azam complex Mbeya city wanapata sare dhidi ya Azam FC, baada ya msimu uliopita kufanikiwa kupata sare ya kufungana goli 3-3