Ijumaa, 10 Juni 2016

HALMAHAURI YA MBEYA YAKAMILISHA UTENGENEZAJI MADAWATI WAMKABIDHI MKUU WA MKOA WA MBEYA AYAGAWE KWA SHULE 51


Halmashauri ya Mbeya imekamilisha utengenezaji wa madawati 5,371 ikiwa ni agizo la Rais kuhakikisha wanafunzi wote wanakaa katika madawati
Akisoma taarifa kwa Mkuu wa mkoa wa mbeya mkurugenzi wa halmashauri Mbeya Viijini Upendo Sanga amesema wamekamilisha utengenezaji madawati mapema kabla ya juni 30 kwenda sambamba na agizo la Mkuu wa mkoa halmashauri zote zikamilishe madawati tarehe 20 juni siku kumi kabla ya tarehe ya mwisho ya mheshimiwa Rais
Mkuu wa Mkoa amekabidhi madawati 3,746 kwa shule 51 na yaliyobaki ameagiza yaendelee kukabidhiwa kwa Shule zingine
Amesisitiza halmashauri zote kukamilisha utengenezaji wa madawati ifikapo tarehe 20 Juni