Ijumaa, 10 Juni 2016

CHUO CHA ILEMI POLYTECHNICS NI JIPU CHAFUNGWA


Katibu mtendaji wa baraza la elimu ya ufundi( NACTE) amewasilisha tamko kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya leo akifunge Chuo cha Mbeya polytechnics kwa kosa la KUDAHILI wanafunzi 270 wasiokuwa na SIFA kati ya wanafunzi 359 wa Chuo hicho .Ni wanafunzi 89 tu ndiyo wana sifa . Wanafunzi hao 270 walidahiliwa kwa ajili ya cheti na diploma ya kilimo wakiwa na ufaulu wa masomo ya sanaa na wengine wakiwa hawana ufaulu wowote
Sababu nyingine ni Chuo kutokuwa na mitaala inliyoidhinishwa na wizara ya kilimo
Kufungwa kwa Chuo hicho kufuatia malalamiko ya wanafunzi kwa Mkuu wa Mkoa wa mbeya mei mwaka huu na Mkuu wa Mkoa kuunda kamati iliyokuwa chini ya mkurugenzi wa NACTE kanda , afisa Elimu wa mkoa na maafisa toka ofisi ya Mkuu mkoa kuiwasilisha taarifa kwa Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa mkoa kuikabidhi kwa Katibu wa NECTA na baada ya kujiridhisha kuwa Chuo hicho nimefanya makosa na kuwasilisha tamko kwa Mkuu wa mkoa na kumuelekeza akifunge Chuo hicho rasmi
Mkuu wa mkoa leo ametoa tamko la kukifunga Chuo hicho na wanafunzi 89 wanahamishiwa Chuo cha Mbalizi polytechinic
Aidha Mkuu wa mkoa ameagiza ada zote zilizolipwa na wanafunzi warejeshewe kwa ajili ya kujiunga na vyuo vingine kwa sifa walizonazo na wakiohamishwa ada yao ipelekwe kwenye Chuo wakuvhohamishiwa wanafunzi hao
Ameagiza jeshi la polisi, mmliki wa Chuo na timu iliyoundwa kuratibu na kutekeleza maagizo hayo kuanzia leo