Ijumaa, 10 Juni 2016

WATUMISHI HEWA 170 WAPATIKANA MBEYA


Serikali Mkoa wa Mbeya imebaini watumishi hewa 170 kutokana na uhakiki ulifanywana timu ya vyombo vya dola iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa mbeya tarehe 20 April mwaka huu na idadi ya watumishi hewa imesababisha hasara ya she 773,882,066

Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya alipokutana na waandishi wa habari kutangaza matokeo ya timu aliyounda kuhakiki watumishi hewa

Pamoja na hasara hiyo watumishi hewa 58 kati ya 170 wamekopa mikopo katika benki jumla ya shilingi 481,574,351

Serikali pamoja na kufanya uhakiki iliwataka watuhumiwa kurejesha fedha zote katika akaunti na sh 65,058,542

Mkuu wa mkoa amewaagiza wakurugenzi kwa kushirikiana na vyombo vya dola kuwasaka popote walipo watumishi hewa na kuwachukulia hatua za kisheria

Aidha amewaagiza wakurugenzi, maafisa utumishi na maafisa wa mfumo kuwajibika kwa kuendelea kulipa watumishi hewa

Kuanzia sasa kila afisa utumishi atawajibika kuwaondoa watumishi watoro pale wanapobainika na amewataka wakurugenzi kuwa na mipango endelevu ya kudhibiti watumishi hewa.