Jumamosi, 9 Aprili 2016

AMOS MAKALA MKUU WA MKOA WA MBEYA ATOA SIKU 14 KWA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA KUAINISHA MIGOGORO YA ARDHI

Mkuu wa Mkoa wa mbeya afanya mkutano wilaya ya Mbarali na kuongea na watumishi wa halmashauri, madiwani, viongozi vyama vya Siasa , viongozi wa dini, wazee maarufu/ machifu, wawekezaji na taasisi za serikali
Ameeleza kuwa Mbarali ni wilaya inayoongoza kwa migogoro ya ardhi na kuletwa kwako Mkoa wa mbeya ni kuhakikisha anashughulikia migogoro ya ardhi na migogoro ya wakulima na wafugaji na katika kuhakikisha migogorovinamalizwa ameagiza yafuatayo
1. Kila kijiji kuwa na matumizi bora ya ardhi
2.viongozi na watendaji kuacha tamaa ya kuuza ardhi na rushwa katika uuuzaji wa ardhi
3. Sheria ya ardhi no 5 ya mwaka 1999 na kanuni zake mwaka 2001 kifungu 8(5) kinazingatiwa kwamba kijiji Hakiwezi kuuza ekari zaidi ya 50 mpaka Mkuu wa wilaya athibitishe na ushirikishaji mkutano Mkuu wa kijijij katika kuazimia uuazaji
4.Kamati za Ulinzi na usalama ngazi zote kuchukua hatua za haraka wanaona viashiria vya migogoro ya ardhi na uvunjifu wa amani
5. Ameagiza semina iitishwe kwa viongozi na watendaji wa Vijiji na kata kuhusiana na sheria ya ardhi na matumizi bora ya ardhi
6. Amewataka wakulima na wafugaji kuheshimiana na kushirikiana kumaliza kwa njia ya amani migogoro inapotikea baina yao
7. Ameagiza Kamati ya Ulinzi na usalama wilaya kuainisha migogoro ya ardhi iliopo katika wilaya na ndani ya siku 14 zoezi hilo likamilike ili ofisi yake kwa migogoro iliyoshindikana ngazi ya wilaya Mkoa ishughulikie na ila inayohitaji ngazi ya wizara aiwasilishe wizara husika