Alhamisi, 11 Juni 2015

WAZIRI MEMBE ATIKISA MBEYA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe jana amepata wadhamini zaidi ya 800 .membe amesema akipata nafasi ya kuteuliwa kuwa mgombea wa urais na hatimaye kuwa rais ,amewahidi wakazi wa mkoa wa mbeya  kuwaongezea  kipato kupitia uwanja wa  ndege wa  kimataifa wa songwe .akielezea maua ,mboga mboga na matunda ,amewashauri wakazi wa mkoa wa mbeya kujenga majengo makubwa ya kuhifadhi maua na mboga mboga.hata hivyo amezungumzia kuhusu  uuzwaji wa mikungu Afrika kusini mkungu wa ndizi ni 15000  wakati mkungu mkoani mbeya mkungu wa ndizi ni 3000 hata hivyo amesema akipata nafasi atawekeza majengo ya usindikaji ili wakulima waweze kuhifadhi vyakula vyao .
membe pia amempa sifa mark mwandosya  kwa kusema ni mtu muadilifu  ,sio mla rushwa  amewambia watu wa mbeya  kuwa kama atashindwa kupata  nafasi  basi yeye atamfanyia kampeni mark mwandosya  na kufanya watu wa mbeya  kumshangilia kwa vifijo na vigelegele pia amezungumzia mikakati ya kuwawezesha wafanyabiashara  wadogo wadogo wakiwemo mama lishe ,bodaboda kuanzisha vikundi vyao na kuanzisha saccos na kuweza kuwasaidia  kukopeshana kwa riba nafuu kabisa na kwa muda muafaka .baadae alipata nafasi ya kukutana na wana vyuo mbalimbali na kuzungumza nao katika hotel ya hill view