Alhamisi, 7 Aprili 2016

Rais Magufuli Arejea Nyumbani Kutoka Rwanda Katika Safari Yake Ya Kwanza Nje Ya Nchi


DIWANI WA KATA YA SISIMBA AJENGA DARAJA LILOKUWA BOVU KWA MUDA WA MIAKA MINGI

DARAJA LINAVYOPITA KIURAHISI KWA SASA MAENEO YA STENDI JIJINI MBEYA
DIWANI WA KATA YA SISIMBA ARI MAARUFU JOFREY KAJIGIRI AKIONGEA NA VYOMBO VYA HABARI JIJINI MBEYA KATIKA MOJA YA HARAKATI ZA USAFI PEMBENI ALIYEVALIA KOFIA NYEKUNDU DIWANI WA SONGWE AYASI NJARAMBAA .

Jumapili, 3 Aprili 2016

AZAM FC YASHIKWA SHATI NA TOTO AFRICA YA MWANZA

KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, imelazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Toto African ya Mwanza, katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) uliofanyika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza jioni ya leo.
Sare hiyo imeifanya Azam FC kufikisha jumla ya pointi 51 ikibakia katika nafasi ya tatu, ikizidiwa pointi mbili na Yanga iliyo nafasi ya pili huku Simba ikiwa kileleni kwa pointi 57, lakini iko mbele kwa michezo miwili dhidi ya wapinzani wake hao.
Mchezo huo uliokuwa wa upinzani kwa pande zote mbili kwa kiasi kikubwa umeharibiwa na mvua kubwa iliyonyesha jijini hapa Mwanza na kufanya uwanja kuloa jambo lililowafanya wachezaji kudondoka chini mara kwa mara na mahesabu ya soka la pasi kushindikana.
Azam FC ndio iliyokuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 23 kupitia kwa nahodha John Bocco ‘Adebayor’ aliyepiga kichwa kizuri kufuatia krosi safi ya Khamis Mcha ‘Vialli’.
Toto Africans ilijipatia bao lake kupitia kwa Wazir Juma dakika ya 40, ambaye alitumia vema makosa yaliyofanywa na beki Pascal Wawa, aliyeruka juu vibaya kuzuia mpira wa kurusha na kuukosa na kufanya kipindi cha kwanza kumalizika kwa timu zote kutoshana nguvu.
Licha ya juhudi za Azam FC kutaka kupata mabao kipindi cha pili kwa kuingizwa washambuliaji Allan Wanga,  Didier Kavumbagu  na kiungo Frank Domayo, na kupumzishwa Farid Mussa na Khamis Mcha, jitihada hizo ziligonga mwamba kufuatia Toto Africans kuingia uwanjani kipindi hicho kwa lengo la kupoteza muda.
Pia hali ya uwanja nayo iliharibu mipango yote ya Azam FC ya kutengeneza nafasi. Hata hivyo waamuzi nao walionekana kuvurunda kwenye baadhi ya matukio kwani hata dakika zilizoongezwa tatu walizoongeza zilishindwa kuendana na namna muda ulivyopotezwa na Toto Africans kipindi cha pili.
Mara baada ya mchezo huo, kikosi cha Azam FC kitaanza safari ya kurejea jijini Dar es Salaam kesho saa 2 asubuhi kwa usafiri wa ndege, tayari kabisa kwa kuanza maandalizi ya mchezo ujao wa ligi dhidi ya Ndanda utakaofanyika Jumatano ijayo (Aprili 6) ndani ya Uwanja wa Azam Complex, Chamazi (Dar).

Jumamosi, 2 Aprili 2016

RAILA ODINGA amtembelea Rais Dkt JOHN MAGUFULI Nyumbani Kwake CHATO

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Kenya Mheshimiwa Raila Amoro Odinga amemtembelea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyopo mapumzikoni katika Kijiji cha Kilimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita.

Mheshimiwa Odinga ambaye ameongozana na mkewe Mama Ida Odinga na Binti yake Winnie Raila Odinga, wametua kwa Helkopta katika uwanja wa Shule ya sekondari ya Chato leo tarehe 02 April, 2016 majira ya saa 11 jioni na baadaye kuelekea nyumbani kwa Rais Magufuli ambako wamepokelewa na wenyeji wao Rais Magufuli mwenyewe na Mkewe Mama Janeth Magufuli.

Akizungumza mara baada ya kuwasili Chato, Mheshimiwa Raila Odinga amesema yeye na familia yake wapo likizo na wamekuja kumtembelea rafiki wa familia yao, kwa lengo la kumsalimia.

"Nimekuja kupumzika na nimekuja na Mama na Mtoto wangu wa kike, na vilevile kuja kutoa pongezi kwa ndugu yangu kwani tangu achaguliwe sijakuja hapa Chato, na nilisema siendi Dar es salaam nitakuja hapahapa Chato" Alisema Mheshimiwa Odinga.

Pamoja na kukutana na Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli, Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya Mheshimiwa Raila Odinga pia amemsalimu Mama wa Rais Bibi Suzana Joseph Magufuli na pia amezulu Makaburi walimozikwa wanafamilia wa Rais, akiwemo Baba Mzazi Mzee Joseph Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimkaribisha Waziri Mkuu mstaafu wa Kenya Raila Odinga nyumbani kwake Chato mkoani Geita mara baada ya Kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikumbatiana na Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Chato Mkoani Geita.
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli mara baada ya kuwasili Chato.
Waziri Mkuu wa mstaafu wa Kenya Raila Odinga akiwa na Rais John Magufuli, Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli pamoja na Mke wa Raila Odinga Bi. Ida Odinga wakisali kwenye makaburi ya familia ya Mhe. Rais Chato Mkoani Geita.
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya Raila Odinga akisalimiana na mama mzazi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Bi Suzana Joseph Magufuli mara baada ya kuwasili Chato Mkoani Geita.

Ijumaa, 1 Aprili 2016

Ewura yashusha bei za umeme service charge nayo yafutwa


Mamlaka ya Usimamizi wa Huduma za Nishati na Maji EWURA imetangaza kushusha bei za umeme kuanzia leo kwa watumiaji wote wa viwango tofauti.

Kushuka huko kwa bei ya umeme ni kutokana na ombi la Shirika la Umeme Tanzania TANESCO kutaka bei za umeme zipunguzwe sambamba na hilo gharama za huduma kwa baadhi ya wateja zimeondolewa.

Bei mpya kwa watumiaji wadogo ni sh.100 kwa uniti, watumiaji wa kati ni sh.292 toka 298 ya zamani.Wafanyabiashara wadogo ni sh. 195 toka sh. 200 ya hapo awali.

Bei mpya kwa wafanyabiashara wa kati ni sh.157 toka sh. 159. Wanaonunua kwa wingi (bulk) ni sh. 152 toka sh. 156 ya hapo awali

Jumapili, 27 Machi 2016

Rais Magufuli Awataka Watanzania kuwa Wamoja


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewasihi watanzania kuendelea kuwa wamoja na kushirikiana kuijenga nchi yao, badala ya kubaguana.

Rais Magufuli ametoa wito huo leo katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Azania Front Jijini Dar es salaam, ambako amesali ibada ya Pasaka pamoja na waumini wa kanisa hilo.

Amesema Mwenyezi Mungu alimtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo kuja kuikomboa dunia bila kuwabagua wanadamu, vivyo hivyo nasi binadamu tunapaswa kutobaguana, iwe kwa dini zetu, makabila yetu, mitazamo ya kisiasa na hata rangi zetu.

Aidha, Rais Magufuli amewakumbusha watanzania kufanya kazi kama ambavyo vitabu vitakatifu vinasisitiza umuhimu wa kufanya kazi, na amebainisha kuwa Tanzania yenye neema inawezekana endapo kila mtu atazingatia kufanya kazi.

“Tukifanya kazi hatuhitaji hata misaada kutoka nje, nchi hii ina neema nyingi. Kwa kweli tukifanya kazi kwa bidi nchi yetu inapaswa kuwa inatoa misaada kwa nchi nyingine na sio kuomba misaada kutoka nchi nyingine” Amesisitiza Dkt. Magufuli.

Rais Magufuli ambaye amesali kwenye kanisa hilo kwa mara ya kwanza tangu achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini ikiwa ni mara yake ya nne kusali katika kanisa hilo hata kabla ya kuwa Rais, amewaomba watanzania kuendelea kuliombea Taifa lao na pia kumuombea yeye ili afanikiwe kutekeleza jukumu kubwa na zito la kuiongoza nchi.

Pamoja na kuongoza maombi ya kumuombea Rais Magufuli na Mkewe Mama Janeth Magufuli waliohudhuria ibada hiyo, Askofu Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Dkt. Alex Malasusa amempongeza Rais Magufuli kwa tabia yake ya kupenda kuhudhuria ibada na kuwasihi viongozi wengine kupenda ibada.

Askofu Malasusa ameuelezea ufufuo wa Yesu Kristo kuwa jambo la kuleta  matumaini, na hivyo amepongeza mwelekeo wa nchi kwa sasa, huku akisema Kanisa linaona matumaini kwa Taifa.

Ijumaa, 25 Machi 2016

MAJIPU KUTUMBULIWA MBEYA


Ni yale ya watumishi waliogawa viwanja vya makazi kwenye vyanzo vya maji Mbozi na eneo oevu Isyesye jiji la Mbeya.

Waliolipana posho za serikali kwenda Dar es Salam kwa ajili ya harambee ya Iyunga sekondari nao kuguswa.

Zaidi ya Milioni kumi zatumika.

WAHUSIKA WA UKUMBI WA MKAPA EBU ANGALIENI UCHAFU ULIOPO NJE YA UZIO WA UKUMBI BASI





Jumatano, 23 Machi 2016

UTATA WAENDELEA KIFO CHA WATU WA TATU WALIOCHOMWA MOTO KYELA MKOANI MBEYA



Hatimaye kitendawili cha watu watatu walionyongwa kisha kuchomwa moto kwenye Gesti ya Mexico mjini Kyela, kimetenguliwa baada ya ndugu kujitokeza na kuwataja kwa majina halisi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi alisema baada ya vyombo vya habari kuandika tukio hilo, ndugu na jamaa wa marehemu walijitokeza na kugundua majina waliyoandika na maeneo wanayotoka ni uongo.

Msangi alisema ndugu wa marehemu baada ya kusoma na kusikia kwenye vyombo vya habari, walianza kuwapigia simu jamaa zao na mmoja wao aligundua kwamba ndugu yake anayeitwa Rogers Mwaka (49), ambaye ni Wakala wa Kampuni ya Vodacom hapatikani na hakuonekana nyumbani.

“Kwa mtandao huo pia tuliweza kufanikiwa kuwapata ndugu wa marehemu wengine, ambao wamewatambua kwa alama na majina yao halisia,” alisema.

Alisema mwanamke aliyeuawa kwenye tukio hilo na kutambuliwa kwa jina la Mariam Hassan, kwa sasa ametajwa kwa majina halisi kwamba ni Zauda Hussein Omary mzaliwa wa Mbarali na mkazi wa Veta jijini hapa wala hatoki Songea.

Msangi alisema marehemu mwingine ametambuliwa kwa jina la Baraka Chaula (27), ambaye ni mdogo wa Zauda kutokana na kuchangia mama, lakini baba tofauti na mkazi wa Mbarali alikuwa akifanya kazi za kilimo na biashara.

Akizungumza kwa uchungu ndugu wa marehemu Zauda na Baraka, aliyejitambulisha kwa jina la Riziki Chaula mkazi wa Mbarali, alisema alifika Kyela baada ya kugundua simu za mdogo wake hazipatikani.

Riziki alisema Zauda ni mke wa Abdallah Malifyuma, anayeishi Mbeya na kwamba alimuaga mumewe kwamba alikuwa akielekea Tukuyu wilayani Rungwe kibiashara.

Mkazi wa Ilomba jijini hapa, Sebastian Amani ambaye alifika Kyela alisema aliamua kupanda gari baada ya simu za Rogers kutopatikana licha ya kuaga kwamba anakwenda Chunya.

Amani alisema chanzo cha mauaji hayo hakijajulikana na kwamba yamewaweka kwenye wakati mgumu jinsi yalivyotokea.

Jana hiyo, Riziki alishirikana na mume wa Zauda, Malifyuma kuchukua miili ya marehemu hao wawili ilhali Aman ‘akibeba msalaba’ wa kusafirisha mwili wa Rogers.

Jumanne, 22 Machi 2016

Chadema wachukua jiji wavunja kambi ya utawala wa ccm


Hatimaye uchaguzi wa Meya wa jiji la Dar es Salaam umekamilika leo katika ukumbi wa Karimjee, na kushuhudia Isaya Mwita wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) akitangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi huo.

Mwita ameibuka na ushindi na kutangazwa kuwa Meya Mpya wa Jiji la Dar es Salaam baada ya kupata kura 84 akimshinda mpinzani wake, Yenga Omary wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) aliyepata kura 67.

Uchaguzi huo umeweka historia ambapo kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi (1992), Chama Cha Upinzani kimepata nafasi ya kuongoza jiji hilo.

Uchaguzi huo uliahirishwa mara kadhaa kutokana na mvutano uliokuwa unaibuka kati ya wajumbe wa CCM na Chadema na kuzua vurugu wakati mwingine.

Tofauti na ilivyo kwa tarehe nyingine za uchaguzi zilizopangwa na kuahirishwa wakati wajumbe wakiwa ukumbini, viongozi wa ngazi za juu wa Chadema pamoja na aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho, Edward Lowassa walihudhuria kushuhudia uchaguzi huo.

Lucy Mayenga Ajisalimisha....Amuomba Rais Magufuli Ampumzishe Ukuu wa Wilaya



Wakati Taifa likisubiri uteuzi wa wakuu wa wilaya huku wanaoshikilia nafasi hizo wakiwa katika chekeche kwa kuzingatia vigezo vitano, Mkuu wa Wilaya Iramba, mkoani Singida, Lucy Mayenga amemuomba Rais John Magufuli asimjumuishe kwenye orodha ya wakuu hao anayotarajia kuitangaza wakati wowote.

Rais Magufuli ameweka bayana vigezo atakavyotumia kufanya uteuzi wa wakuu hao wa wilaya ambavyo ni pamoja na suala la migogoro ya ardhi, tatizo la elimu hasa upungufu wa madawati, njaa na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu alivyovitangaza wakati akizungumza na wazee wa Dar es Salaam na katika uteuzi wa wakuu wa mikoa, alizungumzia pia suala la wafanyakazi hewa ambao wamekuwa wakilipwa mishahara bila ya wahusika kuchukua hatua kudhibiti.

Akizungumza kwenye kikao cha UWT, Mkoa wa Shinyanga mwishoni mwa wiki, Mayenga ambaye pia ni mbunge wa Viti Maalumu alisema aliwasilisha ombi hilo binafsi kwa Rais Magufuli ili apate fursa ya kusimamia biashara zake alizosema zinazodorora kutokana na kubanwa na majukumu ya ukuu wa wilaya.

“Pamoja na ukuu wa wilaya, mimi pia ni mbunge na wakati huohuo ni mfanyabiashara; haya ni majukumu mengi kutekelezwa na mtu mmoja kwa wakati moja,”alisema Mayenga 
Aliwaambia wajumbe waliohudhuria mkutano huo uliofanyika katika Kata ya Nyamilangano, wilayani Ushetu kuwa biashara zake nyingi zilizopo mkoani Shinyanga zimedorora kutokana na kukosa usimamizi wake.

“Ombi hili nililitoa binafsi kwa Waziri Mkuu ambaye alinishauri kusubiri uteuzi; isitafsiriwe kwamba nimeogopa kasi ya utendaji ya Serikali ya Awamu ya Tano.Hapana! Nimeona ni vyema nibaki na ubunge na biashara zangu,” alisema Mayenga ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari.

Baadhi ya wanachama wa UWT waliohudhuria mkutano huo walimpongeza kwa uamuzi huo wakisema unapaswa kuigwa na viongozi wengine wenye majukumu mengi kwa kuachia watu wengine nafasi za kutumikia umma badala ya kung’ang’ania nafasi zote.

“Nampongeza Mheshimiwa Mayenga kwa uamuzi wake wa kuomba asiteuliwe tena kwenye nafasi ya ukuu wa wilaya kwa sababu itatoa fursa kwa watu wengine kutumikia nafasi hiyo,” alisema Selina Mkula.

Katika mkutano huo ambao Mbunge wa Ushetu, Elias Kwandikwa alitoa msaada wa mifuko 60 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa madarasa katika shule za msingi Nyamilangano na Mitonga pamoja na Shule ya Sekondari Kisuke, wanachama wapya 55 walijiunga na UWT.

Mbunge huyo pia aliahidi kutoa vyerehani 20 kwa makatibu kata wa UWT ili kusaidia harakati za maendeleo ya wananchi kwa kuanzisha vikundi vya kiuchumi katika kata zao.

Jumatatu, 21 Machi 2016

Msafara wa Kamati ya Bunge Utawala na TAMISEMI Wapata Ajali Mbaya Bagamoyo ....Watu Watano Wafariki Dunia


 
WATU watano wamefariki dunia huku nane wamejeruhiwa, katika ajali iliyoyahusisha magari manne, mawili yakiwa katika msafara wa Kamati ya Bunge Utawala na TAMISEMI maeneo ya Kerege, Bagamoyo Pwani.

Waliofariki katika ajali ni Hilda Msele (59), Mkuu wa Idara ya Mipango ya Uchumi, Makame Ally (40), Dereva wa Tasaf, Khalid Hassan (40), Tunsime Duncan, Mwanasheria wa Wilaya  na Ludovick Palangya, Mchumi.

Majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Taifa ua Muhimbili ni Ibrahim Matovu, Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Bagamoyo, Juliana Msaghaa, Mhandisi wa Maji wilaya, Dorothy Njetile, Mratibu wa Tasaf, George Mashauri, Mweka Hazina wa Wilaya, Amadeus Mbuta, Mshauri wa Tasaf, Julius Mwanganda, Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii, Tauliza Halidi, Mwananchi na Amari Mohamed, Mwananchi.

Aliyepelekwa katika hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo na kuruhusiwa ni Grace Mbilinyi ambaye ni Afisa Utumishi na Utawala wa Wilaya.

Ajali hiyo ilihusisha lori la mchanga, gari dogo yaliyokuwa yanatokea Bagamoyo kuja Dar es Salaam, na magari mawili yaliyokuwa kwenye msafara wa Kamati hiyo, yaliyokuwa yanaenda Bagamoyo kwa shughuli zake za kibunge.

Magari yaliyokuwa katika msafara wa kamati hiyo, ni gari la Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf) na gari la Mkurugenzi wa Wilaya ya Bagamoyo ambayo yaligongwa na lori hilo la mchanga na kusababisha vifo vya watu hao na kuwajeruhi wengine kadhaa.

Ajali hiyo ilitokea baada ya gari dogo lililokuwa linatokea Bagamoyo kupunguza mwendo ghafla na kusababisha lori lililokuwa nyuma yake kuligonga na kuhama upande wa pili na kuyagonga magari mawili yaliyokuwa katika msafara wa kamati ya Bunge.


==

WATU WATATU WAMEKUTWA WAMEKUFA NYUMBA YA WAGENI HUKO KYELA MKOANI MBEYA


Watu watatu wamefariki dunia kwa kunyongwa na miili yao kuchomwa moto ndani ya nyumba ya wageni iliyopo Wilaya ya Kyela mkoani Mbeya.

Mauaji hayo yamegubikwa na utata kutokana na mazingira ya tukio hilo kuwahusisha wapangaji wa nyumba hiyo usiku wa kuamkia jana.

Mmiliki wa nyumba hiyo iliyopo Mtaa wa Kyela Kati, Boniface Mtengela alisema waliouawa ni watatu kati ya watu wanne waliofika kwa pamoja saa nne usiku jana.

Alisema watu hao walikuwa wanaume watatu na mwanamke mmoja na waliouawa ni mwanamke na wanaume wawili.

Mtengela alisema wanaume wawili walijiandikisha kwa jina la Ali Hassan na mwanamke la Mariam.

“Mwanamume mmoja alipanga chumba namba 14, mwingine 105 na mwenye mke alipanga chumba namba 15.

"Waliokutwa wamekufa ni wanaume wawili wa vyumba na 14 na 105 pamoja na mwanamke huku mwanamume mwenye mke akitoroka,” alisema.

Mganga Mfawidhi wa Wilaya ya Kyela, Francis Mhagama alisema uchunguzi wa miili ya marehemu hao umebaini kuwa waliuawa kwa kunyongwa kisha kuchomwa moto baada ya kumwagiwa mafuta ya taa.

Uchunguzi katika eneo la tukio ulibaini miili yao iliungua, lakini chumba na magodoro havikuungua. Ofisa Mtendaji wa Mtaa wa Kyela Kati, Timoth Luvanda alisema usiku wa tukio hilo hakusikika kelele zozote.

Kamanda wa polisi mkoani Mbeya, Ahmed Msangi hakupatikana kuzungumzia tukio hilo wala kukamatwa kwa mmiliki wa nyumba hiyo na kuhojiwa katika Kituo cha Polisi Wilaya ya Kyela.

Mhudumu wa nyumba hiyo, Hagai Yohana alisema mgeni mmojawapo aliondoka kabla ya saa 12 alfajiri akiwa na kidumu na mfuko wa rambo.

Alisema wageni wote waliandikisha kuwa ni wafanyabiashara na hawakuwa na mizigo.

Ijumaa, 18 Machi 2016

WAZIRI MKUU KUWA MGENI RASMI HARAMBEE YA KUCHANGISHA FEDHA ZA UKARABATI SHULE YA IYUNGA SEONDARI MBEYA

Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika harambee itakafanyika kesho katika ukumbi wa Ubungo Plaza kwa ajili ya kuchangia fedha zitakazowezesha kukarabati mabweni manne ya shule ya Sekondari ya Ufundi ya Iyunga yaliyoungua hivi karibuni.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam,Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe. Nyerembe Munasa Sabi amesema kuwa wameamua kuomba nguvu kutoka kwa wadau wa elimu na watanzania kwa ujumla kujumuika katika kuchangia shule ya sekondari ya ufundi Iyunga ili waweze kukarabati mabweni yaliyoungua kwa moto.

“ Hadi sasa takribani wanafunzi 421 hawana mahala pa kulala kutokana na kuteketea kwa mabweni na kwa kushirikiana na TAMISEMI tumeamua kusitiza masomo kuanzia tarehe11 March hadi tarehe 01 Aprili ili kupisha ukarabati wa mabweni”

“ Tumeanza ujenzi wa baadhi ya miundombinu iliyoteketea na mabweni ikiwa ni jitihada za wadau mbalimbali waliochangia kutoka Mbeya na nawasihi wanambeya wale waliosoma shule ya Iyunga na shule za Mbeya na watanzania kwa ujumla kujitokeza kesho katika harambee hii” Alisema

Mhe. Nyerembe Munasa Sabi aneongeza kuwa wamepokea michango mbalimbli kutoka kwa wadau wakiwemo Mbeya Cement waliotoa mifuko 1,000 ya saruji kwa ajili ya ujenzi na kwa sasa mahitaji yaliyopo ni takribani Shillingi million 770 ili kukarabati na kujenga majengo mapya kwa ajili ya shule hiyo.

Shule ya Sekondari ya  Ufundi Iyunga yenye wanafunzi takribani 9970 kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita imekumbwa na majanga ya moto ambayo yamesababisha athari kwa  watoto kutoendelea na masomo na uharibifu wa miundombinu ila Serikali kupitia TAMISEMI na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mbeya wamejipanga kukusanya  fedha kwa ajili ya ukarabati mkubwa wa shule hiyo.

Jumanne, 15 Machi 2016

KITUO CHA REDIO HUKO TANGA CHATOA TAARIFA ZA UWONGO ZA TFF

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesikitishwa na taarifa za upotoshaji za chombo kimoja cha habari ambacho mmoja wa watendaji alipata fursa ya kuhudhuria mkutano mkuu kama mgeni mwalikwa uliomalizika mwishoni mwa wiki jijini Tanga.
Katika hali inayotia mashaka, siku mbili kabla ya mkutano huo, chombo hicho kiliripoti kuwa wajumbe walikuwa wanalalamika kwa kutopelekewa nyaraka zinazohusiana na mkutano, wakati ukweli ni kuwa nyaraka hizo zilitumwa tangu mwezi Novemba 2015 zikiwa ni sehemu ya barua ya mwaliko wa kikao. Hivyo isingewezekana mwaliko wa kikao ukapokelewa na nyaraka zisiwepo. TFF inao ushahidi wa nyaraka hizo kuwafikia wajumbe wa mkutano huo.
Katika toleo lake la leo chombo hicho kilidai TFF kupata hasara ya shilingi za kitanzania milioni 500.
TFF inaviomba vyombo vya habari kuacha kupotosha juu ya taarifa za mkutano mkuu kuwa shirikisho lilipata hasara (loss) , TFF haifanyi biashara yoyote mpaka kufikia kupata hasara, kilichotokea ni kuongezeka kwa nakisi (deficit) katika bajeti ya mwaka 2014.
Matumizi yaliongezeka kutokana na kulipa madeni ambayo uongozi wa sasa uliyakuta uliyosababisha hata basi la timu ya Taifa likamatwe, kuwepo kwa michezo mingi ya timu za Taifa (Taifa Stars, Twiga Stars, Serengeti Boys), gharama ambazo zilijumuisha kambi za maandalizi za timu pamoja na safari.
Kwa kuwa TFF haifanyi biashara yoyote, matumizi yaliongezeka zaidi ya bajeti iliyokuwa imeratajiwa na kufanya kuwepo na upungufu wa zaidi ya milioni 490.
Aidha TFF imesikitishwa na taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari mwishoni mwa wiki iliyopita, kuhusiana na suala la tiketi za Elektroniki.
Ifahamike kwamba TFF ndiyo ilianzishwa matumumizi ya tiketi hizo kabla hazijasitishwa na Serikali mwaka jana kutokana na kubaini mapungufu katika utekelezaji.
TFF haijawahi kugomea kuwepo kwa mfumo huo wa ki elektorniki, na kwa kushirikiana na Serikali kupitia Wizara ya Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo wanaendelea na mazungumzo juu ya mfumo huo.
Vikao vinaendelea kati ya Wizara na TFF ili kuona njia gani itaweza kutumika katika uendeshaji wa kuingia viwanjani kw aka kutumia mfumo wa ki elektroniki na kesho kutakuwepo na kikao Wizarani kujadili mradi huo.
TFF inatafakari juu ya hatua za kuchukua dhidi ya wanaotoa taarifa za upotoshaji huo.

SHULE YA IYUNGA SEKONDARI YAFUNGWA MBEYA



Uongozi mkoani Mbeya umeifunga Shule ya Sekondari Iyunga baada ya mabweni matatu kuungua moto na wanafunzi kulala nje kutokana na kuyaogopa mabweni yaliyobaki.

Kwa kawaida likizo fupi ilitakiwa kuwa kipindi cha pasaka, lakini shule hiyo ilifungwa Machi 11 hadi 25 na kwamba itaendelea kufungwa hadi Aprili Mosi.

Mkuu wa shule hiyo, Edward Mwantimwa alitoa maelezo hayo kwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jaffo aliyefika shuleni hapo juzi kujionea uharibifu uliotokana na moto uliounguza mabweni matatu kwa nyakati mbili tofauti.

Mwantimwa alisema mara ya kwanza mabweni ya Nyerere na Mkwawa yaliungua Februari 29 na Machi 7 la Shaban Robert, jambo ambalo lilisababisha hofu kwa walimu na wanafunzi na kuanza kuyasusa mabweni mengine.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Nyirembe Munasa akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa alimueleza naibu waziri hatua zilizochukuliwa ikiwamo wadau kutoa misaada na kwamba, pia walikuwa wanaandaa harambee ambayo wangependa ifanyike Dar es Saalaam.

Jaffo alilitaja tukio hilo kuwa ni janga na kuahidi kuwashirikisha wabunge wote kuchangia kurudisha hadhi ya shule hiyo.

“Kuungua kwa shule hii kumeonyesha mengi yakiwamo ya uchakavu wa miundombinu,” alisema.

Alimtaka Nyirembe kusimamia ukarabati wa shule hiyo na uwe umekamilika ifikapo Aprili Mosi.

Jumatatu, 14 Machi 2016

TAKUKURU YAMCHUNGUZA MH LUKUVI NA RUSHWA BILIONI TANO ALIZOKATAA


Takukuru imeanza kuchunguza taarifa kwamba Waziri wa Ardhi, William Lukuvi alikataa kupokea rushwa ya Sh5 bilioni iliyotaka kutolewa na wafanyabiashara wawili wakubwa ili kuwapitishia mradi wa Sh84 bilioni.

Katika mahojiano na gazeti la Mwananchi hivi karibuni, Waziri Lukuvi alisema kwamba lengo la wafanyabiashara hao ilikuwa ni kufanikisha mpango wao wa kuiuzia Serikali ardhi kwa bei kubwa kwenye eneo linalotakiwa kujengwa mji wa kisasa wa Kigamboni.

Licha ya kukataa kutaja majina ya wafanyabiashara hao, Lukuvi alisema mtandao huo wa wafanyabiashara ni hatari na unaweza kusababisha mtu ashindwe kufanya kazi ya wananchi iwapo ataendekeza rushwa.

Jana, Mkurugenzi wa taasisi hiyo, Valentino Mlowola alisema kutokana na taarifa ya kiongozi huyo, ofisi yake iliamua kuchukua chanzo hicho na kuanza kazi ya uchunguzi.

Hata hivyo, Mlowola hakutaka kuweka wazi kazi ya uchunguzi huo imeanza lini wala ilipofikia.

“Kueleza tumeanza lini hilo ni suala la kiufundi, tumeshaanza kushughulikia,” alisema Mlowola ambaye Rais John Magufuli amemuidhinisha rasmi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo baada ya kukaimu kwa miezi kadhaa.

Katika ufafanuzi wake, kamishna huyo wa zamani na mkurugenzi wa Intelijensia ya Makosa ya Jinai katika Jeshi la Polisi, alisema taasisi hiyo kwa sasa imekuwa ikichukua tuhuma yoyote ya rushwa kutoka chanzo chochote baada ya kuripotiwa.

Katika mahojiano hayo, Waziri Lukuvi alisema wafanyabiashara hao waliwaeleza marafiki zake wa karibu kuwa wangempa rushwa.

Mji huo mpya wa Kigamboni unajumuisha kata za Kigamboni, Tungi, Vijibweni, Mjimwema, Kibada, Somangila na eneo lote hilo lina ukubwa wa takribani ekari 6,000.

Awali mradi huo ulitarajiwa kugharimu Sh13 trilioni ambazo zingetolewa na Serikali, lakini ikaamua kushirikisha sekta binafsi ili kuujenga na Serikali ishughulikie uwezeshaji wa awali.

Lukuvi ambaye alihamishiwa Wizara ya Ardhi mapema mwaka jana na kubakizwa katika wizara hiyo na Rais Magufuli, alisema amegundua kuna mtandao mkubwa wa rushwa unaoanzia ngazi ya halmashauri mpaka wizarani ambao unahusisha maofisa wa Serikali na viongozi wa wizara.

“Kama ukiwa na tamaa huwezi fanya kazi uliyotumwa. Kuna wakati walikuja ni wafanyabiashara wawili wakubwa na kutaka wanipe Sh5 bilioni ili nikubali kupitisha mradi wao wa mabilioni ya shilingi na walitangaza kwa marafiki zangu kuwa wangenipa fedha, lakini hapa hawawezi,” alisema Lukuvi.

Aliongeza: “Wakati naingia tu wizara hii nilikuta harakati za kukamilisha mradi wa Kigamboni ukiwa katika hatua za mwisho na kila kitu kilikuwa kimekamilika. Lakini nilipopitia vizuri nilikataa kuwalipa wafanyabiashara hao. Cha ajabu hazikupita siku mbili walipata taarifa wakaja mbio kutaka kuniona.”

Kwa mujibu wa Waziri Lukuvi, wafanyabiashara hao walitaka walipwe Sh141 milioni kwa kila ekari wakati wao walinunua ardhi kutoka kwa wananchi kwa Sh5 milioni kwa ekari, jambo ambalo alisema lilishapitishwa awali.

“Niligundua pale kuna udanganyifu na wizi mkubwa. Haiwezekani mwekezaji anunue kutoka kwa wananchi ekari moja kwa Sh5 milioni, kisha Serikali tumlipe Sh141 milioni kwa ekari kwa kuvuka pantoni tu. Ni wizi mkubwa.

"Kama kweli Serikali ina fedha hizo kwa nini tusimlipe mwananchi moja kwa moja?” alihoji.

Waziri Lukuvi alisema endapo njama hizo zingefanikiwa, Serikali ingetumia zaidi ya Sh84 bilioni kuwalipa wawekezaji hao hewa kwa kuwa mmoja anamiliki takribani ekari 200 na mwingine 400.

“Niliwaambia Serikali haiwezi kuwalipa fedha hizo na badala yake waende kuiendeleza ardhi wenyewe kulingana na mradi unavyotaka. Walitaka kutajirika kwa ujanja ujanja,” alisema Lukuvi na kuongeza:

“Eti walidai wamekopa fedha benki kwa ajili ya mradi huo. Haiingii akilini mtu utumie Sh5 milioni, halafu uje uvune mabilioni ya fedha kwa kuvuka pantoni tu.”

Jumapili, 13 Machi 2016

YANGA SC NA AZAM FC WATAKATA KIMATAIFA


Timu za Azam Fc na Yanga Sc zimefanikiwa kushinda michezo yao ya awali .Yanga walifanikiwa kushinda magoli 2 kwa 1 dhidi APR .nao Azam fc wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao matatu kwa bila.

Ijumaa, 11 Machi 2016

STENDI KUU YA MABASI MBEYA INATISHA MAGUFULI ANGALIA HAYA


STENDI KUU YA MABASI KAMA UNAVYOIONA ILIVYO SASA

HALI NI MBAYA YA JENGO LA KUKALIA ABIRIA WANAOKWENDA MIKOANI JENGO LINAVUJA

JIJI LA MBEYA LINAOMBWA KUKARABATI ENEO ILI KWANI WANACHUKUA USHURU KILA SIKU